
Jeshi la Polisi ZNZ linawashikilia 
watu wawili kwa tuhuma za kuhusika na shambulizi la risasi dhidi ya 
Padri Amros Nkenda(52), mwishoni mwa wiki iliyopita. 
Afisa Habari Mkuu wa Jeshi la Polisi 
ZNZ Inspekta Mohammed Mhina, amesema watuhumiwa hao wamekamatwa usiku wa
 kuamkia leo kwa ushirikiano wa Makachero wa Polisi ZNZ na wenzao kutoka
 PHQ Dsm. 
Bila ya kuwataja majina kwa kuhofia 
kuingilia upelelezi wa kuwapata wengine, Inspekta Mhina amesema 
watuhumiwa hao wanaendeleo kuhojiwa ili kuwapata washiriki wote 
waliohusika ktk njama za kumvamia na kumshambulia kwa risasi Paroko wa 
Parokia ya Mpendae mjini ZNZ. 
Amesema
 bado Makachero hao wa Polisi wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo. 
Jana akizungumza na Waandishi wa Habari ofisini kwake, Naibu DCI ZNZ, 
ACP Yusuf Ilembo, amesema Polisi watahakikisha wale wote waliohusika ktk
 shambulizi hilo wanatiwa nguvuni na kukabili mkono wa sheria. Mwisho.

 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment