Monday 31 December 2012

JESHI LA POLISI LAWASHIKILIA WATU 5 KWA TUHUMA ZA KUHUSIKA NA SHAMBULIO LA RISASI DHIDI YA PADRI AMROS NKENDA



Jeshi la Polisi ZNZ linawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kuhusika na shambulizi la risasi dhidi ya Padri Amros Nkenda(52), mwishoni mwa wiki iliyopita. 
Afisa Habari Mkuu wa Jeshi la Polisi ZNZ Inspekta Mohammed Mhina, amesema watuhumiwa hao wamekamatwa usiku wa kuamkia leo kwa ushirikiano wa Makachero wa Polisi ZNZ na wenzao kutoka PHQ Dsm. 
Bila ya kuwataja majina kwa kuhofia kuingilia upelelezi wa kuwapata wengine, Inspekta Mhina amesema watuhumiwa hao wanaendeleo kuhojiwa ili kuwapata washiriki wote waliohusika ktk njama za kumvamia na kumshambulia kwa risasi Paroko wa Parokia ya Mpendae mjini ZNZ. 
Amesema bado Makachero hao wa Polisi wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo. Jana akizungumza na Waandishi wa Habari ofisini kwake, Naibu DCI ZNZ, ACP Yusuf Ilembo, amesema Polisi watahakikisha wale wote waliohusika ktk shambulizi hilo wanatiwa nguvuni na kukabili mkono wa sheria. Mwisho.

0 comments:

Post a Comment